Biashara ndogo zinaweza kutumia fursa ya huduma za mtandaoni kufikia wateja wengi zaidi. Kuna njia kuu tatu za biashara kuweza kuwafikia wateja wake mtandaoni.

Tovuti

Tovuti inasaidia biashara kutambulika duniani kote, kwani kila mtu mwenye uwezo wa kutumia simu au komputa ataweza kufikia buashara yako bila kufunga safari. Badala ya kupanda gari ya kkoo, mteja anaweza kupitia tovuti yako, ajue unachokiuza, na kununua papo hapo kwa kutumia miamala ya simu.

Matangazo kwenye blog

Tovuti zinazotumika kurusha maudhui mtandaoni yanalenga wasomaji wa rika tofauti. Hizi blog zinaruhusu matangazo kwenye tovuti zao, ambazo ni fursa nzuri kwa mfanyabiashara kuwafikia wateja wengi zaidi.

Mitandao ya Jamii

Mitandao kama ya Facebook na Instagram imeshamiri sana Tanzania, na wafanyabiashara wameona umuhimu wa kurusha maudhui kwenye hii mitandao. Watumiaji wengi hutafuta biashara kwenye Instagram na huangalia picha zilizorushwa kusaidia maamuzi ya kunuua bidhaa husika. Utafiti umeonyesha kwamba biashara zilizoko kwenyemitandao ya jamii zinapata mauzo 78% zaidi ya wenzao wasiotumia hizi huduma.

Ni muhimu sana kwa wafanyabiashara kutambua fursa inayotokana na kutumia huduma za mtandaoni kukuza wigo wa biashara zao, kukuza mapato yao, na kuridhisha watu wengi zaidi na bidhaa zao.

CategoryVidokezo
  1. June 8, 2022

    Hiya, I am really glad I have found this info. Today bloggers publish just about gossips and internet and this is actually irritating. A good site with interesting content, this is what I need. Thank you for keeping this website, I will be visiting it. Do you do newsletters? Can not find it.

    • October 14, 2022

      Hello, thanks for the comment. We post content on the benefits of saving and entrepreneurship. Stay tuned for more.

Write a comment:

*

Your email address will not be published.